Akpan Kusalia Msimbazi.

Kiungo wa klabu ya Simba raia wa Naijeria Vicent Akpan aliesajiliwa kutoka Coastal Union ya mkoani Tanga maarufu kama wanamangushi imeelezwa kua atasalia ndani ya msimbazi.

Kiungo huyo aliesajiliwa mara tu baada ya kumalizika kwa ligi ya Tanzania Bara maarufu kama NBC premier league mwanzo ilisemekana ana uwezekano mkubwa wa kutolewa kwa mkopo baada ya mwalimu Zoran Maki kutoridhishwa na uwezo wake aliounesha katika michezo kadhaa.

Mwalimu Zoran ameeleza atatumia michezo mitatu ya kirafiki inayokuja hapo mbele kumpima mchezaji huyo ili aweze kusalia katika viunga vya Msimbazi. Klabu ya simba inatarajiwa kucheza michezo yake mitatu siku kadhaa mbele ambayo ndo ambayo itatumika kama kipimo cha mwisho cha kiungo huyo kinanaijeria.

Acha ujumbe

Meridianbet
Privacy Overview

This website uses cookies so that we can provide you with the best user experience possible. Cookie information is stored in your browser and performs functions such as recognising you when you return to our website and helping our team to understand which sections of the website you find most interesting and useful.