Chelsea watoa Paundi £ 60M kumsajili Anthony Gordon.

Chelsea walikuwa na ofa ya awali ya takriban paundi £40m-£45m iliyokataliwa na Everton mapema mwezi huu lakini klabu hiyo iko tayari kuongeza ofa yao hadi paundi milioni 60 ili kufanikisha kumpata Anthony Gordon msimu huu wa joto.

Mawasiliano baina ya pande hizo mbili yanaendelea na Chelsea wapo tayari kuongeza ofa yao hadi kiashi hicho walichokitaja kuwa watatoa. Mkataba unabaki mezani kwa Gordon kukubali kwenda Chelsea au vinginevyo ambapo kwa sasa ana mkataba na Everton hadi mwaka 2025.

Frank Lampard anahitaji kuongeza mshambuliaji mmoja kwenye kikosi chake kabla ya dirisha kufungwa, hivyo anategemea mpango wa usajili wa Gordon ukamilike ili apate pesa za kutimiza mipango yake.

Tottenham walitaka kumsajili mchezaji huyo wa kimataifa wa Uingereza kwa mkataba wa mabadilishano na Richarlison kwa jumla ya £80m mapema msimu wa joto lakini hawakufanikiwa. Newcastle pia ilifanya mbinu, lakini haikuwasilisha ombi rasmi.

 

Acha ujumbe

Meridianbet
Privacy Overview

This website uses cookies so that we can provide you with the best user experience possible. Cookie information is stored in your browser and performs functions such as recognising you when you return to our website and helping our team to understand which sections of the website you find most interesting and useful.