Chelsea wanatazamia kutafuta mkataba wa mkopo kwa mchezaji wa Atletico Madrid Joao Felix mwezi Januari.

The Blues wametatizika mbele ya lango msimu huu kwa mabao 17 pekee idadi mbaya zaidi katika nusu ya juu kwenye msimamo wa ligi kuu ya Uingereza.
Na The Telegraph wanadai kuwa watajaribu kusuluhisha tatizo hilo kwa kumnunua nyota wa Ureno Felix kwa mkataba wa awali wa muda mfupi na wajibu wa kumnunua katika majira ya joto.
Wachezaji waliowasili majira ya kiangazi Raheem Sterling na Pierre-Emerick Aubameyang wana mabao manne pekee ya ligi kati yao, huku Kai Havertz hajaonekana kuwa mshambuliaji wa kati anayetegemewa.

Graham Potter pia amempoteza Armando Broja kwa muda wote uliosalia wa msimu huu kutokana na jeraha la ACL alilolipata kwenye mechi ya kirafiki dhidi ya Aston Villa. Felix ametatizika kukidhi bei yake ya pauni milioni 113 katika mji mkuu wa Uhispania na haionekani kuendana na mbinu thabiti ya Diego Simeone.
Lakini uchezaji wake wa Kombe la Dunia kwa Ureno uliviarifu vilabu na kunatarajiwa kuwa na kinyang’anyiro cha kuwania saini yake.

Wapinzani wanne wa juu wa Chelsea, Manchester United na Arsenal pia wanamuwinda na mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 23.

