Chelsea Wavunja Kibubu ili Kumsajili Josko Gvardiol

Chelsea wanatarajiwa kufufua nia yao ya kumnunua mchezaji wa kimataifa wa Croatia Josko Gvardiol Januari hii kufuatia kiwango kizuri kwenye Kombe la Dunia huku vijana hao wa Zlatko Dalic wakitinga nusu fainali nchini Qatar.

 

Gvardiol

Gvardiol bila shaka alikuwa mlinzi bora zaidi kwenye michuano hiyo ikimaanisha kwamba Leipzig wana uwezekano wa kutaka karibu paundi milioni 100 kwa mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 20 wakati soko litakapofunguliwa tena.

Chelsea tayari iliona pendekezo la pauni milioni 77 likitupiliwa mbali mnamo Agosti – ikimaanisha kwamba sasa watalazimika kuongeza ofa yao ikiwa wanataka kufanya makubaliano.

Mchambuzi wa Skysports Merson ana imani kuwa Gvardiol angestahili pesa hizo kwa sababu kwa maoni yake, ndiye beki wa kati chipukizi kutoka kundi dogo la majina.

“Ikiwa Josko Gvardiol hatacheza dhidi ya Lionel Messi basi anaweza kuwa na thamani ya aina hiyo ya pesa,” Merson aliiambia Express Sport pekee.

“Katika siku hizi, hakuna wachezaji wa kati. Ni kama ulimwengu umechukuliwa na mawinga na mabeki wa pembeni.

“Hakuna anayeonekana kutengeneza mshambuliaji wa kati au nusu ya kati tena.”

Real Madrid pia wanaaminika kuwa katika kinyang’anyiro cha kumsajili Gvardiol kutoka Leipzig.

Mchezaji huyo wa zamani wa Dinamo Zagreb alikaribia kujiunga na Leeds chini ya Marcelo Bielsa kwa £15m pekee kabla ya kuhamia Ujerumani. Badala yake, Leeds hatimaye wangemsajili Diego Llorente kutoka Real Sociedad kwa £22m.


Bashiri na kitochi au bila bando mechi hii, Bonyeza hapa kutazama ODDS kubwa na bomba kupitia machaguo spesho ya meridianbet ili kuingia mchezoni. Pia ukibashiri na kitochi kwa dau la TZS 1,000/= Unaweza kuibuka mshindi wa MBUZI WA KITOWEO CHA SIKUKUU, kila wiki Ijumaa.

Acha ujumbe

Meridianbet
Privacy Overview

This website uses cookies so that we can provide you with the best user experience possible. Cookie information is stored in your browser and performs functions such as recognising you when you return to our website and helping our team to understand which sections of the website you find most interesting and useful.