Klabu ya Westham ipo mbioni kumsajili mchezaji wa Aston Villa Danny Ings kwani mpaka sasa wameshatoa ofa ya Euro 12M kwaajili ya kunasa saini ya mchezaji huyo.

Mazungumzo yanaendelea na Ings atakuwa tayari kujiunga na Wagonga nyundo hao wa Uingereza kwaajili ya kuunyesha kile ambacho anacho katika eneo la ushambuliaji kwani mpaka sasa Westham mambo ni magumu.
Danny Ings kabla ya kujiunga na Aston Villa alikuwa akikipiga katika timu ya Southampton ambayo nayo kwasasa bado inajitafuta kutoka katika nafasi ya mwisho kwenye msimamo wa ligi.

Westham ambayo ipo chini ya kocha mkuu David Moyes wamekuwa na msimu mbaya sana kwani mpaka sasa wanashikilia nafasi ya 18 baada ya kucheza michezo yao 19, ushindi mara nne, sare tatu na kupoteza mara 12, wakivuna pointi zao 15.

