Arsenal Yahamisha Majeshi kwa Leandro Trossard

Vinara wa Ligi kuu ya Uingereza Arsenal sasa wamehamia kwenye kumsajili mchezaji wa Brighton Leandro Trossard kwenye dirisha hili dogo la usajili huku mazungumzo tayari yameanza kwa pande zote mbili.

 

Arsenal Yahamisha Majeshi kwa Leandro Trossard

Ofa rasmi kwa mchezaji huyo itakuwa ni mkataba wa kudumu kusalia hapo Emirates huku Trossard akiwa hakucheza mechi iliyopita ya Brighton waliyoshinda dhidi ya Liverpool kwa mabao matatu bila.

Masharti binafsi kati ya Arsenal na mchezaji tayari yameshakubaliwa na yataendelea kwaajili ya mchezaji huyo hatari kutia saini mkataba ndani ya kikosi cha Mikel Arteta.

Arsenal ya Arteta wanawazidi Manchester City ambao wapo nafasi ya pili pointi 8 pekee huku timu hiyo ikitarajia kushuka dimbani leo dhidi ya vijana wa Conte Spurs kwaajili ya kusaka pointi 3 ambazo walizopoteza mechi iliyopita.

Arsenal Yahamisha Majeshi kwa Leandro Trossard

The Gunners wanautaka ubingwa wa EPL ambao hawajaupata kwa muda mrefu na kucheza pia Ligi ya Mabingwa ambayo pia imekuwa kama ndoto kwao. Lakini je wataweza kuhimili kushikilia nafasi hiyo licha ya kuwa mbele pointi nane?

 

 

 

 

Acha ujumbe

Meridianbet
Privacy Overview

This website uses cookies so that we can provide you with the best user experience possible. Cookie information is stored in your browser and performs functions such as recognising you when you return to our website and helping our team to understand which sections of the website you find most interesting and useful.