Chelsea Bado Hali tete Yapigwa Tena

Klabu ya Chelsea bado imeendelea kuchechemea kunako ligi kuu ya Uingereza baada ya kukubali kichapo cha bao moja kwa bila dhidi ya klabu ya Southampton katika dimba lao la nyumbani la Stamford Bridge.

Klabu ya Chelsea imebakubali kichapo cha bao moja kwa bila dhidi ya klabu ya Southampton ambao wanashika mkia kunako ligi kuu ya Uingereza, Bao la mkwaju wa faulo kupitia kiungo wa klabu ya Southampton James Ward Prowse dakika ya 45 ya mchezo na kupeleka kilio darajani.ChelseaSouthampton wao baada ya kushinda mchezo wa leo wanafanikiwa kufikisha alama 18 na unakua mchezo wao wa tano kushinda msimu huu kati ya michezo 23, Baada ya mchezo huu inaweza kua nafasi kwa klabu hiyo kujitengeneza na kutoka mkiani ambapo wapo kwasasa.

Klabu ya Chelsea baada ya kupokea kichapo katika mchezo wa leo klabu hiyo imefikisha mchezo wa sita wa ligi kuu ya Uingereza na kufanikiwa kupata ushindi katika mchezo mmoja  pekee, Kupitia hali inayoendelea ndani ya klabu hiyo ni wazi kua kocha Graham Potter ana wakati mgumu sana kutokana na usajili uliofanyika klabuni hapo.ChelseaChelsea wanaendela kusalia nafasi ya kumi katika msimamo wa ligi kuu ya Uingereza wakiwa na alama zao 31 baada ya kucheza michezo 23 mpaka wakati huu, Klabu hiyo itakua na wakati mgumu sana kuhakikisha wanapata nafasi ya kushiriki michuano ya ligi ya mabingwa ulaya.

Acha ujumbe

Meridianbet
Privacy Overview

This website uses cookies so that we can provide you with the best user experience possible. Cookie information is stored in your browser and performs functions such as recognising you when you return to our website and helping our team to understand which sections of the website you find most interesting and useful.