Mkurugenzi wa klabu ya Juventus Giuntoli amesema kua nyota wa klabu hiyo raia wa kimataifa wa Ufaransa Paul Pogba bado yupo ndani ya klabu hiyo kwakua bado wana mpango nae.
Kiungo Paul Pogba ambaye amekua nje ya uwanja kwa muda mrefu msimu uliomalizika mpaka kuelezwa klabu hiyo ina mpango wa kumpiga bei, Lakini Mkurugenzi Giauntoli amesema bado wana mpango na kiungo huyo msimu ujao.
Mkurugenzi huyo ameweka wazi kwamba bado wanamuhesabu mchezaji kwakua mchezaji huyo bado ni muhimu ndani ya timu hiyo, Hivo ni wazi kiungo huyo wa kimataifa wa Ufaransa ataendelea kuonekana katika jezi ya Juventus.
Taarifa ziliibuka wiki kadhaa zilizopita juu ya Pogba na kusemekana kua klabu ya Juventus imemuweka sokoni kutokana na muenendo wake ndani ya klabu hiyo msimu uliomalizika kugubikwa na majeraha ya mara kwa mara.
Paul Pogba kiungo mwenye ubora mkubwa sana kama anakua kwenye utimamu wake kimwili, Lakini tangu kurejea kwake ndani ya Juventus hakuwafanikiwa kucheza kwa kiwango bora kutokana na majeraha na ndio sababu tetesi za kuondoka klabuni hapo zilizuka.

