Klabu ya Atalanta kutoka nchini ina mpango wa kuwafanyia umafia klabu ya Inter Milan ya nchini Italia pia kwa mshambuliaji Giancluca Scamacca anayekipa West Ham.
Klabu ya Atalanta inataka kutumia faida ya kiwango kidogo cha ofa walichoweka klabu ya Inter Milan cha Euro milioni 24 ambacho inaelezwa West Ham hawajafurahishwa nacho, Hivo hii inaweza kua faida kwao kumpata Scamacca kama watapanda dau.
Klabu ya West Ham wanatarajia klabu ya Atalanta kutuma ofa nzuri zaidi ya Inter Milan, Hivo Inter Milan wasipoongeza kiasi cha pesa watakua kwenye wakati mgumu na huenda wakamkosa mshambuliaji huyo.
Inter Milan mpaka sasa ndio wapo kwenye nafasi nzuri ya kumchukua mshambuliaji Gianluca Scamacca, Lakini kinachowakwamisha ni dau dogo ambalo wameliweka na klabu ya West Ham hawajaridhidhwa nalo.
Mshambuliaji Giancluca Scamacca amefanikiwa kuviingiza vilabu vya Italia kwenye vita kwani kabla ya Inter Milan na Atalanta tayari klabu ya As Roma ilikua inahitaji huduma ya mshambuliaji huyo ambaye ameshindwa kufanya vizuri ndani ya West Ham.

