Rais wa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), Wallace Karia, ametoa onyo kali kwa waamuzi wote watakaoshiriki katika Ligi Kuu ya Tanzania Bara msimu ujao, akieleza wazi kwamba hakuna utaratibu wa kuvumilia makosa makubwa. Aliyasema hayo wakati wa kuitimisha Semina maalumu ya waamuzi iliyofanyikia makao makuu ya TFF, Ilala Dar es Salaam.
“Huu ni msimu tunaotarajia utakuwa tofauti sana, tukimaliza tutapongezana, lakini kwa wale watakaokuwa tofauti tutakuwa tumeachana nao moja kwa moja,” amesema Karia. Aliongeza kuwa hali hii si ya utani na kwamba TFF tayari ina mpango wa kuhakikisha waamuzi wanafuata taratibu za usahihi katika michezo yote ya ligi.

Karia amesema kuwa TFF ipo na utaratibu maalumu kupitia kamati ya waamuzi na paneli ya kujadili utendaji wa waamuzi. “Mwenyekiti wa Kamati ya Usimamizi wa Ligi, kama utaendelea na utaratibu wa kuangalia matukio ya ligi, naomba sana waamuzi ambao mtawaona wana hitilafu, nyie warudisheni katika paneli. Paneli hiyo itafanya kazi yake ikishirikiana na vyombo vingine,” amesema.
Aidha, Karia alikumbusha matukio ya msimu uliopita ambapo makosa ya waamuzi yalisababisha mtikisiko mkubwa nchini hadi kufikia serikali kuingilia kati. Alisisitiza kuwa Tanzania imeshafikisha mpira wake sehemu kubwa ambapo dunia nzima inatambua maendeleo ya ligi, na kwamba ni lazima waamuzi wasiwe chanzo cha kuporomoka kwa soka la nchi.
Bila kusahau meridianbet ndio wakali wa ODDS KUBWA, Machaguo zaidi ya 1000 na kila kitu ukitakacho. Bashiri kijanja hapa


