Kocha mkuu wa Chelsea FC, Liam Rosenior, ameibuka hadharani kumtetea winga wa Real Madrid, Vinicius Jr, kufuatia madai ya kufanyiwa ubaguzi wa rangi katika mchezo wa mchujo wa UEFA Champions League dhidi ya SL Benfica siku ya Jumanne.

Tukio hilo linamuhusisha kiungo wa Benfica, Gianluca Prestianni, ambaye anachunguzwa kwa madai ya kutoa kauli za kibaguzi. Endapo atapatikana na hatia, anaweza kufungiwa angalau mechi 10. Hata hivyo, Prestianni amekanusha tuhuma hizo kupitia taarifa aliyotoa kwenye mitandao ya kijamii, huku uchunguzi ukiendelea.
Bila kusahau meridianbet ndio wakali wa ODDS KUBWA, Machaguo zaidi ya 1000 na kila kitu ukitakacho. Bashiri kijanja hapa

Akizungumza katika mkutano na waandishi wa habari Alhamisi, Rosenior alisema hakuna nafasi ya ubaguzi wa rangi katika soka wala katika jamii kwa ujumla. Alieleza kuwa hawezi kuzungumzia kwa undani tukio hilo kwa kuwa uchunguzi bado unaendelea, lakini alisisitiza kuwa mchezaji anapoonekana kuumia kama Vinicius, mara nyingi huwa kuna sababu ya msingi.
“Nimewahi kufanyiwa ubaguzi wa rangi mimi mwenyewe,” alisema Rosenior. “Unapohukumiwa kwa kitu ambacho unapaswa kujivunia, ni jambo baya sana. Ikiwa mchezaji, kocha au meneja yeyote atapatikana na hatia ya ubaguzi wa rangi, hastahili kuwa sehemu ya mchezo huu.”


