Klabu ya Manchester City ina matumaini ya kumbakisha kiungo wake muhimu Rodri kwa muda mrefu zaidi kwa kumpa mkataba mpya, huku mazungumzo kati ya pande hizo yakiripotiwa kuendelea vizuri.

Kwa mujibu wa taarifa mbalimbali, mabosi wa City wameongeza juhudi za kuhakikisha kiungo huyo wa kimataifa wa Hispania anasaini mkataba mpya licha ya mkataba wake wa sasa kudumu hadi majira ya kiangazi ya mwaka 2027 katika uwanja wa Etihad Stadium.
Bila kusahau meridianbet ndio wakali wa ODDS KUBWA, Machaguo zaidi ya 1000 na kila kitu ukitakacho. Bashiri kijanja hapa

Hata hivyo, Manchester City ilipata matokeo ya sare ya mabao 2-2 dhidi ya Nottingham Forest, matokeo yaliyoiwezesha Arsenal FC kuongeza pengo la uongozi katika msimamo wa Premier League. Katika mchezo huo Rodri alifanikiwa kufunga bao na anaendelea kuonekana kuwa mchezaji muhimu ndani ya kikosi hicho, akitanguliwa na mshambuliaji Erling Haaland kwa thamani ndani ya timu.

Wakati huo huo, Manchester City pia inaelezwa kuwa ina nia ya kumsajili kiungo wa Nottingham Forest, Elliot Anderson, katika dirisha la usajili la majira ya kiangazi, ingawa dili hilo linatarajiwa kuwa na gharama kubwa.

Licha ya tetesi zinazomhusisha Rodri na kujiunga na Real Madrid, taarifa zinaeleza kuwa kwa sasa mazungumzo ya kuongeza mkataba wake na Manchester City yanaendelea, na kuna uwezekano mkubwa kiungo huyo akakubali kubaki klabuni hapo kwa kusaini mkataba mpya.

