Kocha wa Liverpool, Arne Slot, amesema hana majuto yoyote kuhusu maamuzi aliyofanya msimu huu, hata baada ya Mohamed Salah kuthibitisha rasmi kuwa ataondoka Anfield mwishoni mwa msimu. Uhusiano kati ya wawili hao ulitikisika sana mwezi Disemba baada ya Salah kuachwa benchi kwa mechi tatu mfululizo.

Katika kipindi hicho kigumu, Salah alionyesha kutoridhika waziwazi, akidai kuwa klabu ilimtupa chini ya basi wakati timu ikipitia matokeo mabaya. Hata hivyo, Slot amesisitiza kuwa maamuzi yake yalikuwa ya kiufundi na si chanzo pekee cha nyota huyo kuamua kuondoka.
Kocha huyo alieleza kuwa si mara ya kwanza kwa Salah kuachwa nje ya kikosi lakini akaendelea kubaki na kung’ara, akitoa mfano wa matukio ya nyuma chini ya Jürgen Klopp. Kwa hiyo, anapinga dhana kwamba kukosa nafasi kikosini ndiko kumemsukuma mshambuliaji huyo kufanya uamuzi wa kuondoka.

Bila kusahau meridianbet ndio wakali wa ODDS KUBWA, Machaguo zaidi ya 1000 na kila kitu ukitakacho. Bashiri kijanja hapa
Slot pia aligusia kuwa kulikuwa na mazungumzo mengi ya ndani kati ya mchezaji, wakala wake, na uongozi wa klabu kabla ya tangazo hilo kufanyika hadharani. Hata hivyo, alikataa kuweka wazi maelezo ya mazungumzo hayo, akiheshimu faragha ya pande zote husika.

Licha ya tofauti zao, Slot alimsifia Salah kwa mchango wake mkubwa, akiiacha Liverpool akiwa mmoja wa wachezaji bora kuwahi kuivaa jezi hiyo. Akiwa na mabao 255 na makombe makubwa kadhaa.

