Kocha wa Diego Simeone amesema hakuna presha ya ziada kwa Atletico Madrid katika harakati za kutafuta taji lao la kwanza la UEFA Champions League, wakijiandaa kuikaribisha Arsenal kwenye mchezo wa kwanza wa nusu fainali Jumatano.
Atletico wamewahi kufika fainali mara tatu katika historia yao, mbili kati ya hizo zikiwa chini ya Simeone, lakini hawajawahi kutwaa taji hilo. Ni klabu pekee iliyopoteza fainali tatu bila kushinda hata moja, huku pia wakikabiliwa na msimu mgumu ndani ya La Liga wakiwa nafasi ya nne na pointi 25 nyuma ya vinara Barcelona.
Bila kusahau meridianbet ndio wakali wa ODDS KUBWA, Machaguo zaidi ya 1000 na kila kitu ukitakacho. Bashiri kijanja hapa
Akizungumza kuelekea mchezo huo, Simeone alisisitiza kuwa timu yake inaona mashindano hayo kama jukumu, si mzigo.“Hakuna presha, kuna hali ya uwajibikaji na matarajio maalum. Mwisho wa siku huu ni mchezo wa mpira wa miguu na wachezaji ndio wanaoamua matokeo,” alisema Simeone.
Aliongeza kuwa mafanikio yanahitaji juhudi binafsi na si kudaiwa na mashindano.“Mashindano hayamdai mtu chochote. Lazima ujitume, ufanye kazi kwa bidii na kuwa na bahati kidogo ili kufanikisha malengo yako,” alieleza.
Simeone pia alisisitiza kuwa mbinu yao ya kucheza kwa nguvu na kushambulia imekuwa silaha yao kuu katika hatua za mtoano.“Tutaendelea kucheza kwa nguvu, kwa mtindo wetu na kwa kuanzisha mashambulizi. Hivyo ndivyo tutakavyokabiliana na mechi hii,” alisema.
Licha ya ndoto ya kutwaa taji hilo kwa mara ya kwanza, Simeone alisisitiza umuhimu wa vitendo kuliko ndoto.“Kuota ni vizuri, lakini uhalisia ni kile kinachotokea uwanjani. Tuko nusu fainali kwa mara ya nne ndani ya miaka 14, hilo ni jambo kubwa. Tuna matumaini na ari kubwa kuelekea mchezo mgumu ujao,” alihitimisha.

