Beki wa kulia wa Paris Saint-Germain, Achraf Hakimi, atakosekana katika mchezo wa mkondo wa pili wa nusu fainali ya UEFA Champions League dhidi ya Bayern Munich baada ya kupata jeraha la paja, klabu hiyo imethibitisha.
Hakimi alipata jeraha hilo Jumanne wakati PSG iliposhinda mabao 5-4 katika mchezo wa mkondo wa kwanza, ambapo pia alitoa pasi ya bao kwa Khvicha Kvaratskhelia kufunga bao la nne. Licha ya kuumia, mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 27 alimaliza mchezo huo kutokana na PSG kuwa tayari imeshafanya mabadiliko yote.
Bila kusahau meridianbet ndio wakali wa ODDS KUBWA, Machaguo zaidi ya 1000 na kila kitu ukitakacho. Bashiri kijanja hapa
Katika taarifa yake, PSG ilisema, “Hakimi atakuwa nje ya uwanja kwa wiki kadhaa kutokana na jeraha la paja,” hali inayowapa pigo kubwa kabla ya mchezo wa marudiano utakaochezwa wiki ijayo nchini Ujerumani.
Wakati huo huo, kipa Lucas Chevalier naye ameumia paja wakati wa mazoezi ya Jumatano asubuhi, na anatarajiwa kukaa nje kwa muda wa wiki kadhaa pia.
PSG, ambao wanaongoza msimamo wa Ligue 1, wanatarajiwa kuwakaribisha Lorient Jumamosi kabla ya kusafiri kuelekea Munich kwa ajili ya mchezo huo muhimu.
Kocha wa PSG amesema kukosekana kwa wachezaji hao muhimu kutahitaji mbinu mpya, akisisitiza kuwa, “Tunahitaji kujipanga upya na kuhakikisha tunalinda ushindi wetu wa awali.”

