"Jorginho Anafurahia London" Joao Santos

Kiungo wa klabu ya Chelsea, Jorginho “anafurahiwsana” na maisha kwenye Klabu hiyo ya London na hakuna “chochote” kuhusu Mazungumzo ya kuhamia Juventus, wakala wake amesisitiza.

Mchezaji huyo wa Kimataifa wa Italia mwenye umri wa miaka 28 amehusishwa na kuungana tena na kocha wake, Maurizio Sarri huko Turin baada ya miaka miwili na The Blues, ambapo alimsajili kutoka Napoli, Lakini wakala wake Joao Santos amekanusha uvumi, na hata hivyo aligusia kuwa Jorginho anaweza kuongeza Mkataba wake huko Stamford Bridge.

“Juventus? Nilisoma hiyo, lakini sikuwahi kuwasiliana nao, “Wala Sarri wala Fabio Paratici hawajawahi kuniita kwa habari juu ya Jorginho. Hadi leo, sijui kabisa juu ya hali hii.

Jorginho akiwa na Sarri ambaye kwasasa ni kocha wa Juventus

“Anafurahiya sana London, ambapo anaonyesha thamani yake na bado ana miaka mingine mitatu kwenye mkataba wake… Kwa kweli, mnamo Julai, kuna uwezekano wa kuongeza mazungumzo ya Kuongeza mwaka wa nne.. Ndio tutafungua mazungumzo ya mkataba mpya na Chelsea.

“Hatujui mikakati ya usajili wa Juventus ni nini, lakini hii ni mipango yetu kwa siku zijazo. Ninarudia, hadi leo, hakuna Juventus wala timu yoyote nyingine ambayo imejitokeza mbele.”.

2 Komentara

    Anacheza pasi nyingi lakini hazina madhara kwa timu pinzani#meridianbettz

    Jibu

Acha ujumbe

Meridianbet
Privacy Overview

This website uses cookies so that we can provide you with the best user experience possible. Cookie information is stored in your browser and performs functions such as recognising you when you return to our website and helping our team to understand which sections of the website you find most interesting and useful.