Matumaini ya Manchester United kunyanyua ubingwa wa Europa League kwa mara ya pili chini ya kipindi cha miaka minne yalizimwa na Sevilla mnamo Agosti 16, 2020.
Hii ni baada ya miamba hao wa soka ya Uingereza kupokezwa kichapo cha 2-1 kwenye nusu-fainali iliyowakutanisha mjini Dusseldorf, Ujerumani.
Sevilla ambao ni mabingwa mara tano wa Europa League, walitoka nyuma na kusajili ushindi ambao uliwakatia tiketi ya kunogesha fainali itakayowakutanisha na mshindi nusu-fainali nyingine kati ya Inter Milan ya Italia na Shakhtar Donetsk ya Ukraine.

Nusu-fainali hiyo ya pili, ambayo pia itakuwa ya mkondo mmoja pekee, itachezewa nchini Ujerumani mnamo Agosti 17, 2020, siku nne kabla ya fainali kutandazwa Ijumaa ya Agosti 21.
Kiungo mzawa wa Ureno, Bruno Fernandes aliwaweka Man United kifua mbele kupitia penalti ya dakika ya tisa. Ni bao lililowapa ari zaidi huku wakionekana kuwazidi wapizani wao maarifa katika takriban kila idara.
Ingawa hivyo, Sevilla wananolewa na kocha Julen Lopetegui, walisalia imara huku kipa wao Yassine Bounou akifanya kazi ya ziada na kupangua makombora makali aliyoelekezewa na mfumaji Marcus Rashford aliyeshirikiana vilivyo na Fernandes na kiungo Paul Pogba.
Fowadi wa zamani wa Liverpool, Fernandez Saez ‘Suso’ Joaquin alisawazishia Sevilla katika dakika ya 26 baada ya kukamilisha krosi aliyopokezwa na Sergio Reguilon kwa ustadi mkubwa.

Luuk de Jong ambaye ni kiungo wa zamani wa Newcastle United, alikizamisha kabisa chombo cha Man United baada ya kufungia Sevilla bao la pili na la ushindi katika dakika ya 78.
Bao hilo lilitokana na utepetevu wa mabeki wa Man United walioshindwa kudhibiti vilivyo krosi iliyopigwa na nyota wa zamani wa Manchester City, Jesus Navas.
Sevilla walifuzu kwa nusu-fainali baada ya kuwabandua Wolves kwa 1-0 mnamo Agosti 11, 2020. Walifungiwa bao hilo na Lucas Ocampos.
Kwa upande wao, Man-United walitinga hatua ya nusu-fainali baada ya kuwapiga FC Copenhagen ya Denmark 1-0 kupitia penalti ya dakika za mwisho iliyofungwa na Fernandes.

Sevilla ambao kwa sasa wametinga hatua ya nusu-fainali ya Europa League mara saba, wanajivunia rekodi ya kunyanyua ufalme wa Europa League mara nyingi zaidi na wametawazwa mabingwa katika misimu yote mitatu ambayo imewashuhudia wakifika awamu ya robo-fainali.
Drops and Wins!
Umeijua hii? Ni promosheni kabambe ya ushindi kwenye Casino ya mtandaoni ya Meridianbet! Unaweza kushinda hadi Euro 2,000,000 leo.


Latifa juma mohamed
Hongeren Sevilla mmeonyesha ushujaa wenu kwa kuwafunga United.
Ernest
Na kwa taarifa yenu De Gea amefanya makusudi kachoka maana alikuwa anawaokoa sana lakini mwisho wa siku mnasema kiwango chake kibovu kwahiyo jana kasema isiwe tabu najirusha kama nafuata hivi kumbe naachia makusudi
Mwajumah
Hongera sana Sevilla kwa kuwafunga united#Meridianbettz
Sadick
Man ilicheza vzr sana ni kwamba haikuwa na bahati kwa kushindwa kutumia nafasi ilizopata kufunga magoli zaidi na Van Persie alitoa tahadhari mapema kwa man u kutochukulia kirahisi mchezo huo#meridianbettz
Shan
Wanastahili pongezi za dhati.
Lydia Emmanuel Magoti
Ndio mpila ilikuwa akuna jinsi walifosi iliwapate ushindi lakini ndio ivyo imeshindikana
Mwanahamisi
Hongera kwake sevilla
aisha
Sevilla hongera sana kwa kuonesha kipaji chenu maana sio powa wata hawajatarajia
Ester jackson
Kwa kweli man u haikuwa na bahata Jana mana walipata nafasi nyingi kufika kwenye lango LA Seville ila walianbulia patupu na kufungwa 2 ambayo ilikuwa faida ya Seville
Magdalena
united mlijua kutupasua mioyo yetu jana ila hatuna namna maana katika soka kuna matokeo matatu
Khadija
Manchester haina bahati
felister
safi sevila mmejua kunifurahisha
Adelta
Sevilla anastahili pongezi
@meridianbettz
Samiah
Safi Sevilla
Tatu
Mpira kweli unaduka kila MTU akutegemea kama man wanaweza kupigwa kwa timu ndogo kama sevilla hata hvyo man sasa HV wameshuka kiwango
Fatina mfingi
Sevilla jeshi
Issa
Sevilla game ilikuwa upande wao man walishambulia sana lakin bahat haikuwa kwao
Furahav
Daah man u bado.
jullie
tena bado kabebwa hapo
Salma ngende
Kila mtu ana mbabe wake
Gabriel
Hiyo gemu Manchester United waliidharau sana maana Kama nafas walipata nzur sana na walikuwa na nafas nzur ya ushind sema kudharau mechi ndo habar wakaipata maana Kama ukiangalia kiukwel hiyo gem Sevilla alibanwa sana pale alipopata nafas tu alionyesha uwezo wake kiukwelech ilikuwa nzur sana
Fatuma kasomo
Hongera sana sevila
farida ahmadi
Hongera Sana Sevilla
Genia Sikaluzwe
Habari njema kwa mashabiki wa sevilla
Janeflora malisa
Good
Shafii
Matokeo yamekua yakushangaza Sana sivyo Kama watu walivyokua wakitabili ama kweli mpira unamatokeo ya ajabu Sana.
Povel
Sevilla walikuwah kwny ubora Sana ile Jana congrat Sevilla fc
Hope mwaikuka
Man U mmeniboa sana
Sabrina
Man u wameua mkeka wangu niliwapa ushindi wamenikera
Devotha
Hongera sana sevilla
Dorophina
Man u walicheza vizuri tu sema bahati haikuwa yao
Johnmary joel
Sevilla Jeshi kubwa#meridianbett
rama
Maoni:daaaa tumeumia sana mashabiki wa man united
Flomena
Bao hilo lilitokana na utepetevu wa mabeki wa Man United walioshindwa kudhibiti vilivyo krosi iliyopigwa na nyota wa zamani wa Manchester City, Jesus Navas.
Zeiyana
Kwa matokea waliyo kua nayo Manchester united wana panda wana shuka hadi kuja kufikia nusu fainali ilikua kama bahati tu.
Caroline
Niljua tu Sevilla atashinda
Saupha Mohammedans
Man u tunamajonzii
Christa
Waliwakomesha,
David Pere
kwa taarifa yenu De Gea amefanya makusudi kachoka maana alikuwa anawaokoa sana lakini mwisho wa siku mnasema kiwango chake kibovu kwahiyo jana kasema isiwe tabu najirusha kama nafuata hivi kumbe naachia makusudi
warda
Imeniuma sana