Promota wa masumbwi nchini Marekani, Bob Arum ameweka wazi kwamba bondia mtata ambaye pia ni mteja wake, Tyson Fury anapendelea kupata pambano dhidi ya Oleksandr Usyk na sio Dillian Whyte.

WBC bado hawajatoa oda ya pambano la mikanda ya Fury katika kikao chao cha Jumanne usiku, lakini walikuwa wanafikiria kumpatia pambano Whyte baada ya muda mrefu.
Bingwa wa IBF, WBA na WBO Usyk anapamba pambano na marudiano mwaka ujao dhidi ya Anthony Joshua, ambae aliweka kipengele cha pambano la marudiano la haraka.
“Watu kutoka kambi ya Whyte walileta kesi ya usuluhishi dhidi ya WBC. Na WBC walisema hawatatoa nafasi kwa Whyte wakati kuna kesi ya usuluhishi ikiwa inasubiriwa.” Bob Arum aliiambia SkySports.
“Hiyo ni sahihi.
“Fury anaweza kuishia kupigana na Whyte, tutaona.
“Lakini haitakuwa kwa vigezo vya WBC.” aliongeza.
Unasababu milioni za kucheza unavyotaka ukiwa na mabingwa meridianbet, lakini unasababu moja ya kushinda mamilioni katika kasino za mtandaoni za meridianbet. Mchezo maridhawa wa Crazy Time unakupa sababu hizo kuwa mmoja wa washindi leo hii.


