Gary Hoffman ameamua kujiuzuru nafasi yake kama mwenyekiti wa ligi kuu ya Uingereza mwishoni mwa mwezi januari
Uongozi wa ligi kuu ya Uingereza umemshukuru bwana Hoffman kwa kujitoa kwake, kwa kuitumikia taasisi hiyo muda wake wote aliokuwa ofisni kuhakikisha ligi kuu ya Uingereza inapiga hatua.

Gary Hoffman amejiuzuru nafasi ya uenyekiti baada ya matajiri wa Saudi Arabia kuchukua umiliki wa klabu ya Newcastle baada ya bodi kuikubalia “Saudi Public Investment Fund” kuimiliki klabu hiyo huku wakijua kuwa iko chini ya Crown Prince Mohammed Bin Salman.
Klabu 18 za ligi kuu ya Uingereza ispokuwa Newcastle and Manchester City ziliunga mkono kuzuia umiliki na udhamini wa klabu hiyo. Sasa klabu nane za ligi kuu ya Uingereza zinaandaa kanuni mpya amabzo zinatarajiwa kuwasilishwa mwisho huu.

Ikiwa kanuni zinazoandaliwa zitapitishwa basi mkurugenzi wa klabu ya Newcastle Amanda Staveley ambaye kwa sasa anafanya kazi kwa niaba ya Saudia fagio la chuma litampitia.
Uchaguzi wa mwenyekiti mpya unatarajiwa kufanyika haraka iwezekanvyo.
Unasababu milioni za kucheza unavyotaka ukiwa na mabingwa meridianbet, lakini unasababu moja ya kushinda mamilioni katika kasino za mtandaoni za meridianbet. Mchezo maridhawa wa Crazy Time unakupa sababu hizo kuwa mmoja wa washindi leo hii.


