Kocha mkuu wa Coastal Union, Melis Medo na mshambuliaji wa Namungo, Reliants Lusajo wamechaguliwa kama kocha bora na mchezaji bora wa Ligi kuu ya NBC mwezi Desemba.

Kocha Melis Medo amefanikiwa kuwashinda makocha Pablo Franco wa Simba SC na Nasreddine Nabi wa Yanga SC walioingia pamoja katika tatu bora.
Medo alifanikiwa kushinda michezo mitatu na kupoteza mmoja pekee na kupanda kutoka nafasi ya tisa mpaka ya nne katika msimamo wa NPL.
Lusajo alifanikiwa kutwaa tuzo hiyo baada ya kuisaidia timu yake kupanda kutoka nafasi ya 13 mpaka nafasi ya 8 katika msimamo wa NPL wakishinda michezo miwili kupoteza mmoja na sare moja.
Meneja wa Uwanja wa Azam Complex Chamazi, Sikitu Kilakala ametwaa tuzo ya meneja bora wa uwanja wa mwezi desemba kwa mara ya pili mfululizo baada ya kufanya hivyo mwezi Novemba.
Una Kila sababu ya kufurahia wiki yako na kutengeneza mwaka huu uwe wa faida zaidi katika kasino zetu za mtandaoni za meridianbettz. Mchezo wa Zeus Ancient Fortunes unakuongoza kutekeleza hilo.


