Edinson Cavani: Siondoki United Januari Hii

Mshambuliaji wa Manchester United Edinson Cavani amekanusha kuwa anaondoka katika klabu hiyo katika soko la usajili la Januari.

Hivi majuzi kumekuwa na tetesi za uhamisho zinazomhusisha fowadi huyo mzoefu na kuhamia Barcelona mwezi huu, lakini inaonekana sivyo.

Mchezaji huyo wa kimataifa wa Uruguay amecheza mechi nane ndani za Premier League msimu huu, na meneja wa muda Ralf Rangnick sasa amethibitisha kuwa ataendelea kuwepo klabuni hipo hadi angalau msimu wa joto.

Edinson Cavani
Cavani (kushoto) na Rangnick (kulia)

“Nilimwambia kama ingekuwa juu yangu ningemtaka abaki, nikafanya naye mazungumzo. Tulizungumza kwa karibu nusu saa, akaniambia hakika atabaki, na angependa kukaa hadi mwisho wa msimu”

“Sio tu kwa sababu nilimwambia kwamba anapaswa kubaki, alifanya hivyo kwa maamuzi yake mwenyewe, na aliniambia kuwa ninaweza kumtegemea kubaki hadi mwisho wa msimu na kutoa mchango bora zaidi.” -Rangnick juu ya Cavani

Manchester United watakuwa uwanjani Jumatatu katika raundi ya tatu ya Kombe la FA watakapochuana na Aston Villa.


JIACHIE NA ALMIGHTY AZTEC

Ni muda wako kujiachia na mchezo maridhawa wa Almighty Aztec katika kasino bomba za meridianbettz. Nafasi ya kutengeneza mkwanja iko mikononi mwako kazi ni kwako.

tetesi, Tetesi za Soka Barani Ulaya., Meridianbet

CHEZA HAPA

Acha ujumbe

Meridianbet
Privacy Overview

This website uses cookies so that we can provide you with the best user experience possible. Cookie information is stored in your browser and performs functions such as recognising you when you return to our website and helping our team to understand which sections of the website you find most interesting and useful.