Chelsea wamepata taarifa ya bei inayotakiwa kwa mchezaji wa Napoli Victor Osimhen itakuwa £66m.
Uvumi umeenea juu ya mustakabali wa Romelu Lukaku tangu mahojiano yake na Sky Italia kuwekwa hadharani, na mustakabali wake ukihusisha kuondoka kwake, jambo ambalo limesababisha Chelsea kuvutiwa na fowadi huyo wa Naples.
Paris Saint-Germain inasemekana kumtaka mshambuliaji huyo wa Ubelgiji, ingawa ameahidi hadharani kujitolea kwake kwa The Blues kwa sasa, na ameanza mechi mbili zilizopita chini ya Thomas Tuchel.

Hata hivyo, El Nacional wameripoti kwamba Osimhen wa Napoli ana thamani ya £66m na klabu yake ya sasa.
Mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 23 kwa sasa ana kandarasi ya kuitumikia timu hiyo ya Italia hadi 2025, ndiyo maana anathaminiwa sana, huku mshambuliaji huyo akiwa amefunga mara tano kwenye Serie A msimu huu.
Ni muda wako kujiachia na mchezo maridhawa wa Almighty Aztec katika kasino bomba za meridianbettz. Nafasi ya kutengeneza mkwanja iko mikononi mwako kazi ni kwako.

Cheza Hapa

