PSG ni habari ya mjini! Licha ya kutwaa ubingwa wa Ligue 1, hatma ya kocha – Mauricio Pochettino na Kylian Mbappe bado ni kizungumkuti.
Kunafununu kuwa, huenda Pochettino na Mkurugenzi wa michezo – Leornado wakaondoka PSG baada ya msimu huu. Pamoja nao, Kylian Mbappe ananukia kule Santiago Bernabeu wakati huu ambao anamaliza mkataba wake na klabu hiyo.
Maneno na fununu ni nyingi, uhalisia ni upi? Lisemwalo lipo na kama halipo, basi linakuja. Mauricio Pochettino amenukuliwa akisema kuwa, kwa hali ilivyo mpaka sasa – yeye (Pochettino) na Mbappe wataendelea kuwepo klabuni hapo msimu ujao.

Lolote linaweza kubadilika linapokuja suala la usajili wa wachezaji. Real Madrid wanaamini Mbappe atakuwa ni mchezaji wao msimu ujao huku Poch akihusishwa na kurejea Spurs. Hakuna maamuzi yeyote yalifanyika kwa Poch wala Mbappe lakini, kuna uwezekano kukawa na mabadiliko makubwa ndani ya PSG mwishoni mwa msimu huu.
Una Kila sababu ya kufurahia wiki yako na kutengeneza mwaka huu uwe wa faida zaidi katika kasino zetu za mtandaoni za meridianbettz. Mchezo wa Zeus Ancient Fortunes unakuongoza kutekeleza hilo.


