Klabu ya Chelsea ya nchini Uingereza imeongoza kwa kutumia pesa nyingi kwenye usajili msimu huu kwenye majira ya joto, ambapo kwa ujumla imetumia jumla ya $310.2M. Ambapo kwa ujumla ligi ya Uingereza ndio inaongoza kwa kutumia pesa nyingi kwenye usajili kuliko ligi zote tano bora.

Ligi ya Uingereza imetumia takribani kiasi cha $2.2B ikifuatiwa na ligi ya Italy Serie A, ambayo imetumia $749.2M, nafasi ya tatu ikishikiliwa na ligi ya Ufaransa ambayo imetumia takribani $558M, Laliga Santander ikitumia kiasi cha $505M na nafasi ya tano ikishikiliwa na ligi ya Ujerumani ambayo wametumia $484.1M.

Chelsea inaongoza kwenye kutumia pesa kwenye usajili huu kutokana na uhitaji wa wachezaji katika maeneo mbalimbali, ambapo kwenye timu kumi zilizotumia pesa nyingi timu za Uingereza zipo 7.
- Chelsea $310.2M
- Manchester United $261.8M
- Westham United $200.2M
- Tottenham Hot Spurs $186.9M
- Nottingham Forest $178.1M
- Barcelona FC $168.3M
- Psg $162.2M
- Manchester City $153.4M
- Bayern Munchen $151.2M
- Wolveshampton Wonderers $150M
Hizo ni timu kumi zilizotumia pesa nyingi kufanya usajili katika ligi tano bora Duniani mpaka sasa.

