Ligi kuu ya NBC kuendelea kutimua vumbi hii leo, baada ya michezo miwili kupigwa hapo jana. Namungo waliotoka kupoteza mchezo wao wa mwisho watakuwa dimbani kutafuta pointi 3 muhimu dhidi ya Geita Gold.

Wakati huo huo, Geita wao wametoka kupata sare ya bila kufungana kwenye mchezo uliopita dhidi ya Coastal huku wakiwa na hali mbaya baada ya kujinyakulia pointi 7 ndani ya michezo saba waliyocheza, wamepata sare nne, wameshinda mchezo mmoja na wamepoteza michezo miwili kwenye msimamo wapo nafasi ya 13.
Namungo wao wameanza kampeni zao za Ligi kuu vizuri msimu huu huku wakiwa wamepata pointi 11 baada ya kucheza michezo sita, wameshinda michezo mitatu, sare mbili na wamepoteza mchezo mmoja na kwenye msimamo wapo nafasi ya 5 mpaka sasa.

Leo hii wanakutana kwenye uwanja wa Nyankumbu, huku wote wakiwa na uhitaji wa alama hasa kwa mwenyeji kwani kuzikosa hizo alama tatu atazidi kuwa katika hali mbaya sana.
Vijana wa Fred Felix Minziro wakiwa nyumbani kwenye Meridianbet wamepewa ODDS ya ushindi ya 2.05, Sare imepewa 2.65, wakati Namungo wao wamepewa ODDS ya 3.67 lakini pia kunamachaguo mengi zaidi ya 1000 ambayo unaweza kubashiri mechi hii.


