Mzizima Dabi, Azam na Yanga kupigwa Benjamin Mkapa

Klabu ya Azam FC imethibitisha kuwa mchezo wake dhidi ya Yanga SC utachezwa katika Uwanja wa Benjamin Mkapa, Dar es Salaam, badala ya Azam Complex, Jumapili, Machi 15, 2026.

Mzizima Dabi, Azam na Yanga kupigwa Benjamin Mkapa

Afisa Habari na Mawasiliano wa klabu hiyo, Thabit Zakaria ‘Zaka Zakazi’, amesema uamuzi huo umechukuliwa baada ya wamiliki wa Uwanja wa Benjamin Mkapa kuruhusu matumizi yake, huku ukarabati wa Uwanja wa Azam Complex bado haujaanza.

“Kabla ya msimu kuanza, tulichagua kutumia Uwanja wa Benjamin Mkapa kwa mechi zetu mbili za nyumbani dhidi ya Yanga na Simba. Tulipokuwa tukipanga mechi dhidi ya Yanga, tukaangalia uwezekano wa kutumia Uwanja wa Azam Complex, lakini wamiliki wa Benjamin Mkapa walisema kwamba ukarabati haujaanza, hivyo tunaweza kuutumia,” amesema Zaka.

Bila kusahau meridianbet ndio wakali wa ODDS KUBWA, Machaguo zaidi ya 1000 na kila kitu ukitakacho. Bashiri kijanja hapa

Mzizima Dabi, Azam na Yanga kupigwa Benjamin Mkapa

Zaka aliongeza kuwa uwanja huo umewapa Azam FC faida kutokana na rekodi yao ya kushinda Yanga mara nyingi pale, na alihakikisha mashabiki kwamba hakuna hofu ya kukutana na Yanga katika mchezo huo. “Tunaamini tutapata matokeo mazuri,” Kumbuka mchezo wa mwisho wa Ligi Kuu uliochezwa na Azam FC katika Uwanja wa Benjamin Mkapa ulikuwa wa mzunguko wa kwanza dhidi ya Simba SC.

Acha ujumbe

Meridianbet
Privacy Overview

This website uses cookies so that we can provide you with the best user experience possible. Cookie information is stored in your browser and performs functions such as recognising you when you return to our website and helping our team to understand which sections of the website you find most interesting and useful.