Hatma ya Kocha Mkuu wa Chelsea, Liam Rosenior, ipo shakani huku klabu hiyo ikipanga kufanya matumizi makubwa katika dirisha la usajili la majira ya kiangazi, lakini bado haijathibitishwa kama ataendelea kuaminiwa kuongoza mchakato huo.
Kwa mujibu wa taarifa kutoka ndani ya klabu, Rosenior hayupo chini ya presha ya moja kwa moja kwa sasa, lakini vyanzo vimeeleza kuwa nafasi yake inaweza kuwa hatarini iwapo matokeo mabaya yataendelea, hasa baada ya Chelsea kupoteza mechi nne mfululizo na kushindwa kufunga katika michezo mitatu iliyopita.
Bila kusahau meridianbet ndio wakali wa ODDS KUBWA, Machaguo zaidi ya 1000 na kila kitu ukitakacho. Bashiri kijanja hapa
“Hatulaumu mtu mmoja kwa mwenendo wa sasa, lakini tunahitaji kuona maboresho haraka,” kilieleza chanzo cha karibu na klabu hiyo, kikisisitiza kuwa kufuzu UEFA Champions League bado ni lengo kuu la msimu.
Chelsea kwa sasa ipo nafasi ya sita kwenye msimamo wa ligi, na kupoteza tena kunaweza kuziwezesha Brentford na Everton kuipita, hali itakayoongeza presha zaidi kwa benchi la ufundi.
Licha ya Rosenior kusaini mkataba wa miaka sita, inaelezwa kuwa nafasi yake msimu ujao si ya uhakika iwapo mwenendo wa timu utaendelea kuwa mbaya, wakati uongozi wa klabu ukihitaji imani kamili kabla ya kuwekeza fedha nyingi kwenye kikosi.
Chelsea pia inatajwa kupanga kusajili beki wa kati wa kiwango cha juu pamoja na kuongeza nguvu katika nafasi ya kipa, kiungo na ushambuliaji, hatua inayoashiria mabadiliko ya mkakati kuelekea mafanikio ya haraka, huku michezo ijayo dhidi ya Manchester City, Manchester United na Liverpool ikitajwa kuwa ya maamuzi kwa mustakabali wa Rosenior.

