Timu ya Taifa ya Senegal imetwaa ubingwa wa Kombe la Mataifa ya Afrika (AFCON 2021) baada ya kuifunga Egypt 4-2 kwa mikwaju ya penati baada ya dakika 120.
Mechi ya fainali ilichezwa Uwanja wa Olembe jijini Younde, Cameroon ambapo walimaliza dakika 120 bila kufungana na kuamuliwa kwa mikwaju ya penati.
Sadio Mane alikosa penati katika kipindi cha kwanza kabla ya kuja kusahihisha makosa yake na kufunga penati ya ushindi kwa taifa lake na kuipa Senegal ubingwa huo kwa mara ya kwanza katika historia yao.
Kipa wa Chelsea Edouard Mendy alikuwa shujaa wa Senegal, akiokoa penalti ya mchezaji wa akiba Mohanad Lasheen kabla ya Mane kufunga penati yake ya ushindi.
Hii ni mara ya kwanza kwa Simba wa Teranga kutwaa Ubingwa wa AFCON baada ya kucheza jumla ya Fainali tatu za AFCON wakiwa wamecheza mashindano hayo mara 16.
Haijawahi kuwa rahisi hivi kwenye safari yako ya kuvuna mkwanja, kasino maridhawa ya meridianbettz inakuletea mchezo wa Emoticoins unaokupa nafasi ya kufanya safari yako kuwa rahisi zaidi. Wakati ni wako nafasi ni yako na Emoticoins.