Je Singida Big Stars Kulipiza Kisasi Leo?

Ligi kuu ya NBC inaendelea leo kwa michezo miwili huku mchezo wa kwanza utakuwa ni ule unaowakutanisha kati ya Singida Big Stars dhidi ya Azam FC katika uwanja wa Liti huko Singida.

 

Je Singida Big Stars Kulipiza Kisasi Leo?

Mchezo huo utapigwa majira ya 10:00 jioni huku Singida wakikumbuka kupoteza mechi yao ya kwanza walipokutana huko Chamazi na leo ni zamu yao kulipiza kisasi na kusaka pointi 3 wakiwa nyumbani.

Azam wapo nafasi ya tatu kwenye msimamo baada ya kucheza mechi zao 20 wakiwa na pointi zao 43, baada ya kushinda mechi zao 13, sare nne na kupoteza michezo mitatu, huku Walima alizeti wao wakiwa nafasi ya nne, pointi 40.

Je Singida Big Stars Kulipiza Kisasi Leo?

Tofauti kati yao ni pointi tatu pekee, huku mechi 5 za mwisho Wanalamba lamba wameshinda mbili, sare mbili na wamepoteza moja. Vijana wa Pluijm wao wameshinda nne na sare moja.

Acha ujumbe

Meridianbet
Privacy Overview

This website uses cookies so that we can provide you with the best user experience possible. Cookie information is stored in your browser and performs functions such as recognising you when you return to our website and helping our team to understand which sections of the website you find most interesting and useful.