Klabu ya Singida Big Stars imefanikiwa kuifunga klabu ya Kagera Sugar kwa bao moja kwa bila katika mchezo wa ligi kuu ya NBC uliopigwa katika dimba la Liti Mkoani Singida.
Klabu ya Sigida Big Stars imefanikiwa kupata alama tatu muhimu kwenye mchezo huo wakiwa katika dimba lao la nyumbani leo mapema leo. Mchezo huo ambao ulikua mgumu zaidi lakini klabu hiyo ya walima alizeti walifanikiwa kupata matokeo mazuri.
Klabu ya Kagera Sugar wo walifanikiwa kupambana katika mchezo huo kuhakikisha wanapata alama tatu , Lakini haikuwezekana kutokana na miopango ambayo walikua nayo vijana wa Hans Van Der Pluijm kuhakikisha klabu hiyo inapata alama tatu.
Klabu ya Singida Big Stars baada ya kupata alama tatu muhimu kupitia bao pekee lililofungwa na kiungo wao Bruno Gomes imefanikiwa kufikisha alama 40 kwenye ligi kuu ya NBC huku ikishika nafasi ya nne kwenye msimamo wa ligi hiyo.
Klabu ya Kagera Sugar wao wanashindwa kupata matokeo mazuri katika mchezo wa pili mfululizo kwani mchezo uliomalizika walipata alama moja, Huku mchezo wa leo wakifungwa bao moja kwa bila na kuwafanya kusalia kwenye nafasi kwenye msimamo wa ligi kuu wakiwa na alama 24.

