Mchezaji mpya aliesajiliwa na klabu ya Yanga Mamadou Doumbia anayecheza nafasi ya beki, ametua Dar es salaam leo hii alfajiri kwaajili ya kujiunga na wenzake na kuwatumikia wananchi.

Mamadou ambaye ni raia wa Mali ametokea katika kambi ya timu ya Taifa hiyo inayoshiriki michuano ya CHAN nchini Algeria.
Yanga wanaendelea na mazoezi yao kujiandaa na mchezo wao wa ligi kuu utakaopigwa siku ya Jumatatu ambapo watamenyana dhidi ya Ruvu Shooting ambao wapo nafasi ya 15 kwenye msimamo.

Wachezaji wote wa Yanga waliosajiliwa kabla ya dirisha dogo la usajili kufungwa wapo kambini kwaajili ya kujiandaa na kusaka pointi tatu na kuhakikisha wanatetea tena taji lao la ligi kuu kwa mara ya pili mfululizo.

