Kocha wa Manchester United, Michael Carrick amesema kuwa mchezo dhidi ya Liverpool unabaki kuwa wa kipekee licha ya timu hizo kutokuwa kwenye mbio za ubingwa wa Premier League msimu huu. Timu hizo mbili zenye mafanikio makubwa nchini England zinatarajiwa kukutana katika dimba la Old Trafford siku ya Jumapili.
Carrick alieleza kuwa mchezo huo ni miongoni mwa mechi anazozipenda zaidi kutokana na historia na ushindani uliopo kati ya klabu hizo mbili. “Bila shaka huu ni mmoja wa michezo ninayoipenda sana, ni mchezo wa kipekee. Kuna michezo mikubwa na ushindani mwingine, lakini huu uko juu kabisa,” alisema.
Bila kusahau meridianbet ndio wakali wa ODDS KUBWA, Machaguo zaidi ya 1000 na kila kitu ukitakacho. Bashiri kijanja hapa
Alisisitiza kuwa historia, ushindani na hisia kali vinaufanya mchezo huo kuwa wa kipekee kwa mashabiki na wachezaji.
“Historia yake, matokeo ya nyuma, msisimko na burudani pamoja na hisia zinazohusika vinafanya huu kuwa mchezo maalum sana,” aliongeza Carrick.
Kocha huyo wa zamani wa United alisema timu yake imepiga hatua kubwa tangu msimu uliopita walipomaliza nafasi ya 15 kwenye msimamo wa ligi, pointi 42 nyuma ya mabingwa Liverpool.
“Hii inaonyesha maendeleo ya kikosi chetu na namna tunavyozidi kuwa imara. Tunaingia kwenye mchezo huu tukiwa katika nafasi nzuri na matokeo mazuri,” alisema.
Carrick pia alieleza kuwa licha ya tofauti ndogo ya pointi kati ya timu hizo kwenye msimamo wa ligi, hawazingatii sana hilo kabla ya mchezo huo. “Tunatambua hali ya ligi na jinsi ilivyo karibu, lakini huu ni mchezo wa kipekee, hatuuchukulii kama mingine,” alifafanua.
Aidha, Carrick alifurahishwa na kiungo Kobbie Mainoo kusaini mkataba mpya wa miaka mitano, akieleza kuwa ana mchango mkubwa katika kikosi. “Amefanya vizuri sana na bado ana mengi ya kuonyesha. Ni kijana mdogo lakini yuko kwenye kiwango kizuri kwa sasa,” alihitimisha.

