Simba Yaingia Mkataba na MO Bima.

Klabu ya Simba leo imeingia mkataba na Kampuni ya Bima ya MO Assuarance wa kuigharamia katika masuala ya Afya na matibabu ya wachezaji wa Simba, Simba Queens, Benchi la Ufundi, wafanyakazi wote wa klabu hiyo na Familia zao.

Simba Yaingia Mkataba na MO Bima.

Kupitia C.E.O wao Barbara Gonzalenz amesema kuwa; “Leo tunaingia rasmi kwenye ushirikiano na Mo Assurance kama mshirika rasmi wa bima wa Simba SC”.
Lakini pia aliongezea kwa kusema ushirikiano huo ni mzuri kwani utawawezesha wachezaji pamoja na familia zao kupata huduma hiyo kwa haraka zaidi.
Mkataba huo ni wa miaka miwili wa bima ya afya kwa wachezaji, benchi la ufundi na menejimenti ya Wekundu wa Msimbazi na kampuni ya Bima ya MO Assuarance kwa kipindi cha miaka miwili wenye thamani ya Tsh. 250 milioni.
Mkurugenzi mtendaji wa MO Assuatance Gregory Fortes, amesema kuwa wao kama kampuni wameamua kutoa bima ya afya, huku kukiwa na aina tofauti kama watu wanaolazwa, wanaokwenda kutibiwa na kurudi nyumbani kwao na mambo mengine madogodogo kama matatizo ya meno, macho lakini pia wameongeza huduma ya majeraha yanayotokana na michezo.
Simba Yaingia Mkataba na MO Bima.
Lakini pia Afisa habari na mawasiliano wa klabu hiyo Ahmed Ally amesema kuwa ili mtu apate ufanisi  kwenye kufanya kazi ni lazima awe huru kwenye malazi, yeye mwenyewe kuugua au watu wanaomzunguka. Sasa ili kuwafanya wafanyakazi wa Wekundu wa Msimbazi kuwa wenye ufanisi wao, leo wamewaletea bima ya kushughulika na afya zao.

Acha ujumbe