Baada ya kutoa sare ya kufungana mchezo uliopita dhidi ya Mbeya City, klabu ya Simba imewasili Moshi kucheza mchezo wao mwingine wa ligi dhidi ya Polisi Tanzania ambao wapo na hali mbaya.

Simba ilisafiri jana kuelekea Moshi kuzisaka alama tatu ambazo wameshindwa kuzipata huko Sokoine na kusababisha kuwa na gepu kubwa kati yao na wapinzani wao wakubwa Yanga.
Polisi baada ya kucheza michezo 13 amejipatia pointi 11 tu huku akiwa na idadi kubwa ya mechi alizopoteza zikifikia nane, ushindi mara mbili na sare tatu huku akiwa nafasi ya 14 hadi sasa.
Simba wao wapo nafasi ya tatu kwenye ligi baada ya sare iliyopita sare nne, ushindi mara nane na kupoteza mara moja huku akiwa na mlima mrefu wa kutetea taji kutokana na kuwa na sare nyingi.

Je Polisi Tanzania wataweza kupata ushindi wa tatu kwa Simba ambao kama mbio za ubingwa zinaanza kupotea kutokana na kuwa wameachwa pointi kadhaa na Yanga ambao wana michezo miwili mkononi.
Je wewe hucheza Kasino Mtandaoni na umekuwa ukijiuliza ni mchezo gani rahisi na mzuri kwa ushindi? Basi Usihangaike Aviator ni rahisi zaidi kucheza na kushinda, kingine cha zaidi ni kwamba Aviator Bonanza imerudi tena Cheza zaidi ujiweke kwenye nafasi ya kushinda Samsung A23.
BONYEZA HAPA KUCHEZA


