Klabu ya Aston Villa imefikia makubaliano na Bayer Leverkusen ya kumsajili winga wa klabu hiyo, Leon Bailey kwa makubaliano yaliyoripotiwa ya pauni milioni 30 (€ 35m) katika majira haya ya kiangazi.

Makubaliano hayo yamefikiwa baina ya pande zote mbili, na dili liko mbioni kukamilika huku vipimo vya afya pekee vikiwa vimesalia kabla ya kutangaza rasmi.
Bailey, 23 ametumikia klabu hiyo ya ujerumani kwa miaka minne na nusu kabla ya kuamua kutafuta changamoto mpya na kukubali kujiunga na Villa.
Taarifa kwenye wavuti rasmi ya Villa inasomeka: “Aston Villa na Bayer Leverkusen wamefikia makubaliano ya uhamisho wa Leon Bailey chini ya mchezaji kukamilisha matibabu na kumaliza masharti ya kibinafsi.”
SHOOT! mchezo unaokupa nafasi ya kupambania ushindi wako mkubwa kwenye kasino ya mtandaoni ya Meridianbet! Usisubiri hii, jiunge sasa kufurahia ushindi!



Sania+mapua
Habari njema