Paris Saint-Germain wanafikiria kumnunua mshambuliaji wa Chelsea Pierre-Emerick Aubameyang wa Chelsea msimu wa dirisha dogo linaloanza Januari, na mchezaji huyo mpaka sasa ana miaka 33.

Aubameyang alijiunga na Blues msimu huu wa dirisha kubwa baada ya miezi saba tuu kuondoka Arsenal na kwenda kujiunga Barcelona katika dirisha la usajili la Januari. Ripoti kutoka Ufaransa zinasema kuwa tayari mazungumzo yanaendelea kuhusu mchezaji huyo kuhamia kwa wababe hao wa Ligue 1 msimu ujao wa joto.
Aubameyang ambaye ni raia wa Gabon anaanza kupata muunganiko mzuri ndani ya Chelsea huku akifunga mabao yake katika mechi zake mbili za hivi karibuni dhidi ya Crystal Palace na AC Milan.

Nahodha huyo wa zamani wa Arsenal alisajiliwa katika dakika za mwisho, huku kocha wa zamani Thomas Tuchel akidhaniwa kuwa ndiye aliyehusika na uhamisho wa mshambuliaji huyo. Mjerumani huyo ambaye alimpisha Graham Potter ambaye huenda akaunga mkono maono ya Boehly kwa kutenegeneza kikosi cha vijana.

