Kocha mkuu wa AC Milan Stefano Pioli ameitaka timu yake kujibu kichapo cha jumatano walichokipokea cha mabao 3-0 dhidi ya Chelsea katika michuano ya klabu bingwa watakapowakaribisha Juventus katika mchuano mkubwa wa Serie A leo hii.

Mabao kutoka kwa Wesley Fofana, Pierre-Emerick Aubameyang na Reece James yaliiangamiza Milan waliokuwa Stamford Bridge katika hatua ya makundi ya Ligi ya Mabingwa na Milan kusalia nafasi ya tatu.
Milan wamefanya vyema zaidi kwenye ligi ya Serie A ambapo mpaka sasa wapo nafasi ya 5 huku wakiachwa nyuma pointi 3 tuu na kinara ambaye ni Napoli. Pioli akiongea kwenye mkutano na waandishi wa habari na kutaka timu yake iweke kando kupoteza kwao mchezo wao wa klabu bingwa.

“Tuliweka mchezo wa London nyuma yetu mara moja na tutaurudia kuanzia Jumapili na kuendelea,” Pioli alisema. “Wachezaji wana hamu ya kujibu”. “Hii haimaanishi kuwa tutashinda kwa sababu wapinzani wapo pia, lakini hatutakosa hamu, ari na dhamira.
Kocha huyo amesema kuwa wameruhusu mabao machache sana na wanaweza kufanya vizuri zaidi. Chelsea ilifanya vyema kutumia makosa yao .

