Klabu ya Brighton imepoteza mechi ya pili mfululizo toka kuondoka kwa Graham Potter dhidi ya Brentford hapo jana walipokuwa ugenini na walipoteza kwa mabao 2-0.

Mpaka sasa hiyo inakuwa ya pili baada ya kupoteza mechi iliyopita dhidi ya Spurs wakiwa nyumbani. Mabao hayo yalifungwa na Ivan Toney katika vipindi vyote vya mchezo na kuifanya Brentford isogee hadi nafasi ya 8 kwenye msimamo.
Brighton mambo yanakuwa si mambo huku siku si nyingi mchezaji wake muhimu Mwepu amestaafu kutokana na matatizo ya moyo sasa klabu inaanza kupoteza nguvu huku kukiwa na ujio wa kocha klabuni hapo ambae ni Roberto De Zerbi.

Mechi inayofuata klabu hiyo itamenyana na Nottingham Forest kabla ya kuja kuumana na Manchester City Oktoba 22. Mwalimu ana kazi ya ziada ya kufanya kikosini hapo kutokana na mabadiliko ambayo yametokea.

