Klabu ya Chelsea imeshinda Kombe la Dunia ngazi ya vilabu kwa mara ya kwanza baada ya Kai Havertz kufunga mkwaju wa penalti katika muda wa ziada na kuwafanya kupata ushindi mnono wa 2-1 dhidi ya Palmeiras ya Brazil mjini Abu Dhabi.
Bao la 10 la Romelu Lukaku msimu huu liliifanya Chelsea kuwa na matumaini ya kuhitimishwa haraka katika jitihada zao za kukamilisha kazi safi ya kutwaa mataji makubwa ya kimataifa ya vilabu.
Lakini Palmeiras walikuwa na mawazo mengine na mkwaju wa penalti wa Raphael Veiga ulipeleka pambano hilo hadi dakika za nyongeza kwenye Uwanja wa Mohammed Bin Zayed.
Thiago Silva aliadhibiwa kwa kushika mpira wa mkono na mkwaju wa penati uliopigwa na Veiga, kabla ya Chelsea kuzawadiwa penati katika dakika 30 za nyongeza na kutwaa ubingwa huo.
Haijawahi kuwa rahisi hivi kwenye safari yako ya kuvuna mkwanja, kasino maridhawa ya meridianbettz inakuletea mchezo wa Emoticoins unaokupa nafasi ya kufanya safari yako kuwa rahisi zaidi. Wakati ni wako nafasi ni yako na Emoticoins.