EPL, bodi ya ligi kuu ya Uingereza imepanga kubadilisha kanuni za kuihilisha mechi kutokana na mlipuko wa Uviko-19, klabu itapaswa kutoa ushahidi wa angalau wachezaji wanne wenye maambukizi ili kuweza kuomba kuhirishwa kwa mchezo huo.
Kutokana na wimbi jipya la Uviko-19, ligi kuu ya Uingereza imeathiliwa na kirusi hicho na kusababisha kuahirishwa kwa michezo kadhaa kwa wiki za hivi karibuni, michezo kadhaa imeahirisha kwa takribani wiki sita au zaidi.
Waraka huo kutoka bodi ya ligi ya uingereza EPL umeandikwa kama ifuatavyo:-
“Kufuatiwa na kikao kilichofanyika hivi leo na vilabu, bodi ya ligi imetoa muongozo kuhusu uhailishwaji wa mechi kutokana na Uviko-19 kuwa kikwazo cha michezo kuendelea, kuanzia sasa ikiwa klabu itaomba kuahirishwa kwa mchezo, kutokana na idadi ya wachezaji kutotosha ni lazima wawe na wachezaji wanne wenye maambukizi kwenye kikosi.
Muongozo huu utaanza rasmi kwenye mchezo wa ligi kuu unaofwa tarehe 5 february siku ya jumamosi kwenye mchezo kati ya Burnley vs Watford.
Dakika tano pekee zinakutosha kuwa mmoja wa washindi wa mkwanja mrefu ndani ya kasino pendwa ya meridianbettz katika sloti maridhawa ya KENO, moja ya michezo inayoipa thamani dau lako.