Mshambuliaji wa Klabu ya AS Vita, Fiston Mayele amekiri kwamba ana marafiki wengi katika klabu ya Yanga ya Tanzania ambao walikuwa wakicheza pamoja katika klabu hiyo.
“Kunipata mimi ni kutokana na wao kuwasajili Djuma, Mukoko na Tuisila. Hawa ni marafiki zangu sana, tumecheza nao hapa AS Vita kwa wakati tofauti, timu ya namna hiyo utagundua kwamba inataka mafanikio”,
“Huwa naongea nao sana, wananiambia kwamba wananisubiri nije hapo, najua watu wa hapo wanataka mtu anayejua kufunga, maneno ambayo hata kocha (Nabi) ameniambia pia,”
“Sina wasiwasi na kazi yangu. Najua kufunga. Hapo kuna viungo wazuri sana ambao tukisaidiana kwa pamoja ni rahisi kufanikiwa Nafurahi pia kuona timu itakuwa inashiriki mashindano ya Afrika,” Fiston Mayele
Ndio, kama bado hujajiunga na Familia ya Mabingwa ya Meridianbet, huu ndio wakati wako! Tunakupatia Bonasi ya 3,500 Tsh papo hapo kama sehemu ya ukaribisho!


