West Ham Wanataka Kumsajili Beki wa Kulia wa Manchester United Wan-Bissaka

West Ham United wanataka kumsajili beki wa kulia wa Manchester United Aaron Wan-Bissaka kwa mkopo katika dirisha la uhamisho la Januari.

 

wan-bissaka

Wan-Bissaka, 24, amecheza dakika nne pekee msimu huu na mara ya mwisho alianza kwa United katika kichapo cha 1-0 dhidi ya Everton mnamo Aprili 9. Alianza kwa mara ya kwanza chini ya Erik ten Hag katika kipigo cha kirafiki dhidi ya Cadiz mnamo Desemba 7.

United ilimfahamisha Wan-Bissaka kuwa yuko huru kuondoka kabla ya mwisho wa msimu uliopita na kulikuwa na nia ya West Ham katika majira ya joto.

West Ham United wanataka kumsajili beki wa kulia wa Manchester United Aaron Wan-Bissaka kwa mkopo katika dirisha la uhamisho la Januari.

 

wan-bissaka

West Ham wako nafasi ya 16 kwenye Premier League na meneja David Moyes amekuwa na wakati mgumu kupata mlinzi wa kawaida wa kulia.

Mabeki wa kulia wanaotambulika Vladirmir Coufal na Ben Johnson, wameanza takribani idadi sawa ya michezo ya ligi huku Thilo Kehrer aliyesajiliwa majira ya kiangazi, beki wa kati akipangwa katika safu ya beki wa kulia katika mechi tatu zilizopita za ligi.

United ilimnunua Wan-Bissaka kwa £45m iliyopanda hadi £50m kutoka Crystal Palace Julai 2019 lakini ameshindwa kuwa beki wa kulia mwenye uwezo wa kushambulia na nafasi yake iliporwa na Diogo Dalot Desemba mwaka jana.

 

wan-bissaka


Bashiri na kitochi au bila bando mechi hii, Bonyeza hapa kutazama ODDS kubwa na bomba kupitia machaguo spesho ya meridianbet ili kuingia mchezoni. Pia ukibashiri na kitochi kwa dau la TZS 1,000/= Unaweza kuibuka mshindi wa MBUZI WA KITOWEO CHA SIKUKUU, kila wiki Ijumaa.

Acha ujumbe