Mkali wa mchezo wa tenisi kutoka nchini Marekani, Serena Williams amepigwa faini ya dola za Kimarekani 17,000 (takribani shilingi milioni 39 za Kitanzania ) kwa vitendo vya utovu wa nidhamu alivyofanya kwenye fainali ya michuano ya US Open iliyopigwa New York nchini Marekani mwishoni mwa wiki iliyopita.
Moja ya matukio yaliyochangia Serena Williams kupigwa faini hiyo ni mabishano haya aliyoyafanya dhidi ya mwamuzi akimtuhumu kuwa ni mbaguzi wa jinsia na mwizi.
Kwenye mtanange ule Naomi Osaka aliweka historia ya kuwa Mjapan wa kwanza kushinda taji hilo baada ya kumshinda Serena Williams kwa seti 6-2, 6-4.


