Mshambuliaji wa klabu ya PSG kylian Mbappe inaelezwa atakua nje ya uwanja kwa muda wa takribani wiki tatu hivo kumfanya kuukosa mchezo muhimu wa ligi ya mabingwa ulaya dhidi ya Bayern Munich.
Mshambuliaji Kylian Mbappe alionekana kuchechemea katika mchezo ambao PSG walipata ushindi wa mabao matatu kwa moja hapo, Lakini hapo mwanzo ilionekana kua jeraha hilo haliwezi kua na tatizo kubwa sana lakini mpaka sasa inaoneakana atakua nje kwa muda.
Mshambuliaji wa huyo ni wazi ataukosa mchezo wa ligi ya mabingwa barani ulaya dhidi ya klabu ya Bayern Munich katika hatua ya 16 bora utakaochezwa mwezi huu wapili kutokana na taarifa ambayo imeeleza kua mchezaji huyo atakua nje ya uwanja kwa muda wa miezi mitatu.
Mbappe atakua nje kwa muda wa wiki tatu ambapo atakosa mchezo wa kwanza wa hatua ya 16 bora dhidi ya Bayern Munich kwenye ligi ya mabingw abarani ulaya, Lakini taarifa nzuri ni kua mchezaji huyo atakosekana katika mchezo wa awali tu lakini mchezo wa marudiano utamkuta staa huyo akiwa tayari amerejea.
Kukosekana kwa mshambuliaji Kylian Mbappe ndani ya klabu ya PSG kwa muda wa wiki tatu ndani ya klabu hiyo ni pengo kubwa licha ya klabu hiyo kua na mastaa kadhaa kama Messi, na Neymar lakini umuhimu wa mchezaji huyo ni mkubwa sana ndani ya timu hiyo, Zaidi kwenye mchezo muhimu dhidi ya Bayern Munich.

