Neville: Messi Kwenda Marekani Utakua Usajili wa Kihistoria

Gwiji wa zamani wa klabu ya Manchester United, Everton na timu ya taifa ya Uingereza Phil Neville amesema nyota wa klabu ya PSG Lionel Messi akijiunga na ligi kuu ya Marekani utakua usajili wa kihistoria.

Phil Neville ambaye kwasasa ni kocha wa klabu ya Inter Miami inayoshiriki ligi kuu nchini  Marekani maarufu kama MLS anaamini ujio wa Lionel Messi kwenye ligi kuu ya Marekani utakua na mvuto wa ajabu na utaweka historia kubwa.NevilleLionel Messi ambaye anakipiga ndani ya miamba ya soka nchini Ufaransa kwasasa anawindwa na klabu ya Inter Miami kwa kiasi kikubwa, Inaelezwa klabu hiyo inamuwinda staa huyo tangu dirisha lililopita na bado wako tayari kumshawishi dirisha kubwa linalofata.

Kocha Phil Neville anaona pia sio mbaya kwa mchezaji huyo kujiunga na ligi kuu Marekani kwani atakua anafuata nyayo za wachezaji wenzake wakubwa mbalimbali ambao wamewahi kupita ligi kuu ya Marekani kama Andrea Pirlo, Steven Gerrard, David Beckham, na Zlatan Ibrahimovic.NevilleKlabu ya PSG ipo mezani na nyota Lionel Messi kwajili ya kumuongezea mkataba mpya staa huyo hivo klabu ya Inter Miami itakutana na ushindani mkali kutoka kwa wababe wa ligi kuu ya Ufaransa, Lakini mwisho wa siku mchezaji huyo ndio ataamua hatma yake kusalia PSG au kutimkia MLS.

Acha ujumbe

Meridianbet
Privacy Overview

This website uses cookies so that we can provide you with the best user experience possible. Cookie information is stored in your browser and performs functions such as recognising you when you return to our website and helping our team to understand which sections of the website you find most interesting and useful.