Yanga Yalamba Milioni 10 za Mama Samia Jana

Klabu ya Yanga imelamba tena Milioni 10 za mama Samia hapo jana baada ya kuikandamiza Real Bamako mabao 2-0 katika Dimba la Benjamin Mkapa.

 

Yanga Yalamba Milioni 10 za Mama Samia Jana

Mabao hayo ya ushindi yalitupiwa kimyani na mshambuliaji Fiston Mayele katika dakika ya 08 ya mchezo pamoja na Jesus Moloko katika dakika ya 68 ya mchezo huku Bamako wao mambo yakizidi kuwaendea kombo.

Baada ya ushindi huo wa jana Yanga wapo nafasi ya pili baada ya kukusanya pointi zao 07, huku kinara wa kundi hilo akiwa ni US Monastir ambaye alishinda pia jana na kufikisha pointi 10.

Yanga Yalamba Milioni 10 za Mama Samia Jana

Mechi inayofuata atamenyana dhidi ya US Monastir huku mechi ya mwanzo walipokutana vijana wa Nabi walipoteza wakiwa ugenini. Baada ya kupoteza mechi ya jana Bamako wanazidi kushikilia mkia.

 

 

Acha ujumbe

Meridianbet
Privacy Overview

This website uses cookies so that we can provide you with the best user experience possible. Cookie information is stored in your browser and performs functions such as recognising you when you return to our website and helping our team to understand which sections of the website you find most interesting and useful.