Imani ya Klopp Leo

Klabu ya Liverpool inayoongozwa na meneja Jurgen Klopp ina imani kwamba watakuwa imara zaidi wakati wanapokwenda kumenyana na wapinzani wao wakubwa Tottenham ambayo ni mechi ya mapema zaidi leo hii Ligi Kuu ya Uingereza!

Hii ni mara baada ya ndege ya kukodishwa kuwasafirisha wachezaji watatu wa pale Anfield kutoka Brazil ambao ni Roberto Firmino, Alisson na Fabinho kutoka Marekani ambapo walikuwa wanachezea timu ya taifa lao hilo.

Watatu hao waliwasili kwa wakati na kushiriki mazoezi na wachezaji wengine siku ya Alhamisi wiki hii kwa mujibu wa Daily Mirror. Jurgen Klopp anatarajiwa kuimarisha zaidi benchi lake la wakufunzi klabuni Liverpool kwa kumuongeza kocha wa makipa wa timu ya taifa ya wachezaji chipukizi Jack Robinson wa Uingereza ambaye alifanya kazi Manchester United kwa miaka 7.

Kete yako unaitupa wapi? Usipitwe na gemu hii na nyingine nyingi kukujia.

Acha ujumbe