Milan wamevijulisha vyombo vya habari kuwa kutakuwa na hafla ya kumpigia saluti Zlatan Ibrahimovic kesho huko San Siro, kwani mkataba wake hautaongezwa, lakini maisha yake ya Serie A yanaweza kuendelea.

Mshambuliaji huyo anatimiza umri wa miaka 42 mwezi Oktoba na mkataba wake wa sasa unatarajiwa kumalizika Juni 30.
Ilikuwa imedhihirika kwa muda kwamba labda asingeendelea na uchezaji wake na Rossoneri baada ya msimu uliotawaliwa na matatizo ya majeraha. Ameweza kucheza mechi nne pekee za Serie A msimu huu, akifunga bao moja, katika jumla ya dakika 144 za soka.
Huku Zlatan akiwa majeruhi tena kesho dhidi ya Hellas Verona, kutakuwa na hafla fupi mwishoni mwa mechi ambayo mshambuliaji huyo wa Sweeden anaweza kuwapigia saluti mashabiki kwenye viwanja.

Ilikuwa ni tetesi, mchana wa leo Milan walivijulisha vyombo vya habari vinavyoangazia mchezo huo kuhusu muda wa tukio hilo, na kuthibitisha kwa hakika kwamba Ibrahimovic hataongeza mkataba wake.
Alicheza jezi ya Milan mara mbili, kuanzia 2010-2012 na akarejea Januari 2020, akicheza mechi 163 za ushindani akiwa na mabao 93 na asisti 35. Katika klabu hiyo, Ibrahimovic alishinda mataji mawili ya Serie A na Supercoppa Italiana.
Huu unaweza usiwe mwisho wa kazi yake, ingawa, kwasababu Monza ana nia ya kumleta mkongwe huyo kwenye Uwanja wa U-Power.

Itakuwa ni muungano tena, ikizingatiwa Monza inaendeshwa na wakuu wa zamani wa Milan Silvio Berlusconi na Adriano Galliani.

