Uongozi wa Yanga SC kupitia Eng. Hersi Said umesisitiza msimu huu una jambo lao na kwamba hawana muda wa kubembeleza mchezaji, kama akipigiwa simu halafu asipokee au akikosa mechi ajue namba inachukuliwa na wengine.

Hayo yamewekwa wazi na mjumbe wa Kamati ya Mashindano ya Yanga SC, Hersi Said alipokuwa akihojiwa ambapo alisema hawana nafasi ya kumbembeleza mchezaji kama atashindwa kufuata matakwa na miongozo ya timu kwa sasa kikosini.
“Nyie si mmeona kuna mchezaji juzijuzi alifunga bao akamwaga machozi, si mmeona wenyewe. Hakuna anayetaka kupoteza nafasi yake kikosini,” alisema Hersi.
“Yanga SC inalipa mishahara yenyewe. Ina mifumo yake ya kuajiri watu sisi tunasapoti tu. Yanga ni timu kubwa huwezi kufananisha na wengine. Huwezi kumleta mchezaji kama Bangala (Yanick) halafu hajui mshahara analipwa na nani.” aliongeza.
Mkwanja umetema ndani ya kasino za meridianbettz, Mchezo maridhawa wa Aurora Beast Hunter unakupa nafasi sawa ya ushindi leo hii, kila mzunguko una nafasi ya kuibuka mshindi, na mkwanja wako unaupata kila mzunguko utakapo kamilika.


