Ligi Kuu ya NBC Tanzania Bara, imeendelea kuthibitisha hadhi yake barani Afrika baada ya kutajwa rasmi miongoni mwa Ligi 10 Bora kwa mujibu wa Shirikisho la Kimataifa la Historia na Takwimu za Mpira wa Miguu (IFFHS). Kwa takwimu zilizotangazwa hii leo, Ligi Kuu ya NBC imeorodheshwa nafasi ya sita (6) kwa ubora barani Afrika, huku ikishika nafasi ya 54 duniani.
Kwa upande wa Afrika, Ligi Kuu ya NBC imeshuka kwa nafasi mbili ikilinganishwa na mwaka 2024, lakini bado imeendelea kusalia ndani ya orodha ya ligi bora zaidi barani humo. Hata hivyo, kimataifa Ligi hiyo imepiga hatua kubwa kwa kupanda nafasi tatu duniani, kutoka nafasi ya 57 mwaka 2024 hadi nafasi ya 54 mwaka 2025.


